Amda Iyasus
Mandhari
Amda Iyasus (alifariki Juni 1434) alikuwa Mfalme wa Ethiopia kwa kipindi cha mwaka mmoja, kuanzia 1433 hadi 1434. Alijulikana kwa jina la kiti cha enzi Badel Nan na alikuwa mwanachama wa Solomonic dynasty. Alikuwa mtoto mdogo wa Takla Maryam.[1]
Kulingana na E. A. Wallis Budge, Amda Iyasus alitawala kwa miezi nane tu, na hakubaki na watoto. Vyanzo vya kifalme pia havielezei matendo yake wakati wa utawala wake mfupi. Al-Maqrizi aliripotiwa kushangazwa na mzunguko wa haraka wa wafalme waliotawala.[2]
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ British Museum. Dept. of Oriental Printed Books and Manuscripts; William Wright (1877). Catalogue of the Ethiopic Manuscripts in the British Museum Acquired Since the Year 1847. British Museum. ku. 7–.
- ↑ Budge, A History of Ethiopia: Nubia and Abyssinia, 1928 (Oosterhout, the Netherlands: Anthropological Publications, 1970), p. 303.
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Amda Iyasus kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |