Nenda kwa yaliyomo

Alda Lara

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Alda Ferreira Pires Barreto de Lara Albuquerque anajulikana kama Alda Lara (alizaliwa tarehe 9 juni 1930, Benguela, Angola hadi 30 Januari 1962, Cambambe, Angola) ni mshairi wa Angola anayetumia lugha ya kireno.[1][2]

Maisha ya awali na elimu

[hariri | hariri chanzo]

Alda Lara alizaliwa tarehe 9 juni 1930 katika mji wa Benguela, Angola. Alitokea katika familia ya kitajiri na alipata elimu ya Kikristo, ambayo ilimpa uhuru wa nafsi kulingana na mchambuzi. Kaka yake alikuwa mshairi mashuhuri aliyeitwa Ernesto Lara Filho . Lara alisoma katika shule ya wanawake huko (kwa sasa inafahamika kwa jina la Lubango) Sá da Bandeira, kabla ya kuhamia Ureno kumaliza shule ya sekondari. [3] Alisoma katika Chuo Kikuu cha Lisbon na akaishi katika Nyumba ya Wanafunzi wa Dola. Alikuwa mwanafunzi mwenye bidii na alianza kazi yake ya uandishi kwa kuchapisha mashairi katika jarida la kifasihi Mensagem, chapisho mahususi kwa Waafrika. Baadaye Lara alienda kusoma katika Chuo Kikuu cha Coimbra na kupata digrii katika masuala ya dawa.[4]

  1. "Alda Lara". Nação Ovimbundu.org (kwa Portuguese). Iliwekwa mnamo 6 Novemba 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unrecognized language (link)
  2. Margaret Busby (ed.), Daughters of Africa: An International Anthology of Words and Writings by Women of African Descent from the Ancient Egyptian to the Present, London: Jonathan Cape, 1992; Vintage, 1993.
  3. "Biografia de Alda Lara". Lusophonia Poetica (kwa Portuguese). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 7 Novemba 2016. Iliwekwa mnamo 6 Novemba 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unrecognized language (link)
  4. Sheldon, Kathleen (2016). Historical Dictionary of Women in Sub-Saharan Africa (tol. la 2nd.). Rowman & Littlefield. uk. 155. ISBN 978-1442262935.