Albinus wa Angers

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Albinus akishiriki Mtaguso wa tatu wa Orleans.

Albinus wa Angers (kwa Kifaransa: Aubin; Vannes, leo nchini Ufaransa, 496 hivi - Angers, 1 Machi 550) alikuwa kwanza mmonaki, halafu abati kwa miaka 25 na hatimaye askofu wa mji huo kuanzia mwaka 529[1], akijitahidi kurekebisha Kanisa kufuatana na mtaguso wa tatu wa Orleans na kutetea fukara na wafungwa hata kwa kukemea vikali fahari ya matajiri[2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[3].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Machi[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

THE LIFE OF ST. AUBIN by Venantius Fortunatus, translated by John Dodd

THE MIRACLES OF ST AUBIN by Nicholas Belfort, translated by John Dodd

THE LIFE OF ST AUBIN – DETAILS ON SOURCES by John Dodd

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.