Alberto wa Sarteano
Mandhari
Alberto wa Sarteano (Sarteano, 1385 - Milano, 15 Agosti 1450[1]) alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo na kasisi wa Kanisa Katoliki.
Alijiunga na urekebisho wa Waoservanti mwaka 1415 akashirikiana hasa na Bernardino wa Siena akawa makamu wa mkuu wa shirika lote [2]. Pamoja na Yohane wa Kapestrano na Yakobo wa Marka, hao wawili ndio wanaohesabiwa nguzo ya tawi hilo.
Kutokana na sifa yake kubwa, anaheshimiwa kama mwenye heri.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 15 Agosti.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |