Alberta Ampomah
Mandhari
Alberta Boatema Ampomah (alizaliwa 3 Novemba, 1994 mjini Accra) ni mwanamichezo wa kuinua uzito kutoka nchini Ghana. Alimuwakilisha Ghana katika Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Joto mwaka 2012 yaliyofanyika London, Uingereza.
Pia amewakilisha Ghana katika mashindano ya kuinua uzito katika kundi la wanawake wa kilo 75 katika Michezo ya Madola ya mwaka 2010 yaliyofanyika Delhi, India. Aliweka nafasi ya tatu katika kipengele cha clean and jerk katika mashindano ya kuwania tiketi za Olimpiki Afrika, lakini alipewa nafasi ya kipekee (wild card) ya kushiriki katika Michezo ya Olimpiki.[1][2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Alberta Ampomah". Sports Reference. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 18 Aprili 2020. Iliwekwa mnamo 7 Januari 2014.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Ghana Weightlifter Hopes To Win Olympic Medal". Peace FM Online. 17 Julai 2012. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 31 Januari 2013. Iliwekwa mnamo 5 Agosti 2012.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Alberta Ampomah kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |