Ainsley Maitland-Niles
Mandhari

Ainsley Cory Maitland-Niles (alizaliwa 29 Agosti 1997) ni mchezaji wa soka wa kulipwa kutoka Uingereza anayocheza nafasi ya kiungo mkabaji au beki wa kulia katika klabu ya Lyon inayoshiriki Ligue 1.
Maitland-Niles alitumia msimu wa 2015–16 kwa mkopo katika Ipswich Town, akitokea Arsenal. Pia alitumia nusu ya pili ya misimu ya 2020–21 na 2021–22 kwa mkopo katika West Bromwich Albion na Roma, mtawalia.
Katika msimu wa 2022–23, alicheza kwa mkopo katika Southampton, kabla ya kujiunga na Lyon baada ya mkataba wake na Arsenal kumalizika.
Katika ngazi ya kimataifa, ameiwakilisha England kuanzia timu ya chini ya miaka 17 hadi timu ya taifa ya wakubwa.[1][2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://www.ol.fr/en/football/roster/players/ainsley-maitland-niles
- ↑ https://www.thefa.com/england/mens-seniors/squad/ainsley-maitland-niles
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ainsley Maitland-Niles kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |