Ahabu

Ahabu (kwa Kiebrania: אַחְאָב, Aẖ'av, ʼAḥʼāḇ), mwana wa Omri, alikuwa mfalme wa saba katika ufalme wa Israeli. William F. Albright alikadiria utawala wake kuwa miaka 869–850 KK, E. R. Thiele miaka 874–853 KK[1] na Michael D. Coogan miaka 871–852 KK.[2].
Vitabu vya Wafalme vinamchora kama mwovu sana, kwa kufuata mke wake Yezebeli, kumuua Naboti na manabii mbalimbali na kuelekeza taifa la Israeli kuabudu miungu mingi, hasa Baali. Lakini Nabii Elia kwa karama yake ya kutokea na kutoweka hakuweza kuuawa kama manabii wenzake wengi, akafaulu kuokoa imani katika Mungu pekee, YHWH. Kazi yake ilikamilishwa na mwanafunzi wake, nabii Elisha aliyempaka mafuta Yehu awe mfalme na arudishe Israeli kwa Mungu wake. Katika mapinduzi ya Yehu, Yezebeli aliuawa kikatili (2Fal 9:1-36) kama alivyotabiri Elia.
Habari zake zinasimuliwa hasa katika Kitabu cha Kwanza cha Wafalme, 16-22.
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Edwin Thiele, The Mysterious Numbers of the Hebrew Kings, (1st ed.; New York: Macmillan, 1951; 2d ed.; Grand Rapids: Eerdmans, 1965; 3rd ed.; Grand Rapids: Zondervan/Kregel, 1983). ISBN 0-8254-3825-X, 9780825438257.
- ↑ Michael D. Coogan, A Brief Introduction to the Old Testament, (Oxford: Oxford University Press, 2009) 237.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- Achtemeier, Paul, mhr. (1996). The HarperCollins Bible Dictionary. New York: HarperCollins.
- Coogan, Michael David (2009). A Brief Introduction to the Old Testament: The Hebrew Bible in Its Context. Oxford: University Press. ISBN 978-0-19-533272-8.
- Craig, James A. (1887). "The Monolith Inscription of Salmaneser II". Hebraica. 3 (4): 201–232. doi:10.1086/368966. JSTOR 527096.
- Cook, Stanley Arthur (1911). . Katika Chisholm, Hugh (mhr.). Encyclopædia Britannica. Juz. la 1 (tol. la 11th). Cambridge University Press. ku. 428–429.
{{cite encyclopedia}}: Cite has empty unknown parameter:|coauthors=(help) - Finkelstein, Israel; Silberman, Neil Asher (2002). The Bible Unearthed: Archaeology's New Vision of Ancient Israel and the Origin of Sacred Texts. Simon and Schuster. ISBN 978-0-7432-2338-6.
- Thiele, Edwin Richard (1965). The Mysterious Numbers of the Hebrew Kings: A Reconstruction of the Chronology of the Kingdoms of Israel and Judah. Paternoster Press.
- Ussishkin, David (2010). "Jezreel–Where Jezebel Was Thrown to the Dogs". Biblical Archaeology Review. 36 (4).
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Ahab Ilihifadhiwa 14 Februari 2009 kwenye Wayback Machine.—Archaeowiki.org
| Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ahabu kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |