Afro-Shirazi Party

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kanga ikitangaza TANU na ASP (makumbusho ya House of Wonders, Stone Town, Zanzibar).
Historia ya Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
This article is part of a series
Uendo
Historia ya Zanzibar
Afrika Mashariki 1800-1845
Ukoloni
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland
Mkwawa
Vita vya Maji Maji
Vita vikuu vya kwanza Afrika Mashariki
Tanganyika
Mapambano ya uhuru Tanganyika
Uhuru
Uhuru wa Tanganyika
Mapinduzi ya Zanzibar
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Julius Nyerere
Ujamaa
Tamko la Arusha
Vita vya Kagera
Ali Hassan Mwinyi
Benjamin Mkapa
Jakaya Kikwete
John Magufuli
Samia Suluhu Hassan

Tanzania Portal

Afro-Shirazi Party (kifupisho: ASP) kilikuwa chama cha siasa cha Zanzibar. Kilianzishwa mwaka 1957 kwa muungano kati ya Shirika la Washirazi (Shirazi Association) na Shirika la Waafrika (African Association). Shirika la Shirazi (lililoanzishwa 1939) lilikuwa muungano wa Waafrika wazalendo wa Unguja na Pemba, Shirika la Waafrika (lililoanzishwa 1934) muungano wa Waafrika wenye asili ya bara, pamoja na asili kati ya familia za watumwa wa awali kutoka bara na wafanyakazi waliohamia katika karne ya 20.

Chama kilikuwa na wafuasi wengi kisiwani Unguja, ilhali sehemu ya Washirazi wa Pemba walipigia kura vyama vingine.

Katika uchaguzi kabla ya uhuru mwaka 1963 ASP ilipata asilimia 54.2 za kura lakini, kutokana na mfumo wa uchaguzi, haikupata wabunge wengi, hivyo serikali ya kwanza baada ya ukoloni ilianzishwa na vyama vya ZNP na ZPFP.

Katika Januari wa 1964 kikundi cha wana ASP wenye silaha kilichoongozwa na John Okello ilipindua serikali ya Sultani wa Zanzibar pamoja na kuua wakazi wengi Waarabu na Wahindi na kuunda serikali ya kimapinduzi chini ya urais wa Abeid Karume[1].

Mwaka wa 1977, ASP iliungana na TANU kuwa Chama cha Mapinduzi.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Mohammed Ali Bakari, The Democratisation Process in Zanzibar: A Retarded Transition, Hamburg ; Institut fur Afrika-Kunde , 2001.

(Hamburg African Studies ; ISBN 3-928049-71-2; ISSN 0947-4900 (online hapa)