Afrika ya Kati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Africa ya Kati)

Afrika ya Kati ni kanda la bara la Afrika iliyoko katikati ya bara. Katika hesabu ya Umoja wa Mataifa (UM) nchi 9 zifuatazo huhesabiwa kuwa sehemu zake:

Afrika ya Kati

Jina la nchi au eneo,
bendera
Mji Mkuu
Angola
Luanda
Kamerun
Yaoundé
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Bangui
Chadi
N'Djamena
Kongo, Jamhuri ya
Brazzaville
Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia
Kinshasa
Guinea ya Ikweta
Malabo
Gabon
Libreville
São Tomé na Príncipe
São Tomé

Afrika ya Kati kwa maana ya mpangilio ya UM ni nchi kusini ya jangwa Sahara, mashariki ya Afrika ya Magharibi na upande wa magharibi wa Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki. Mto mkubwa wa kanda ni mto Kongo.

Mwisho wa ukoloni kati ya 1953-1963 palikuwa na Shirikisho la Afrika ya Kati la nchi za kisasa za Malawi, Zambia na Zimbabwe zinazohesabiwa siku hizi kuwa sehemu za Afrika ya Kusini au Afrika ya Magharibi.