Édith Piaf

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Édith Piaf
Édith Piaf

Edith Piaf (19 Desemba 191511 Oktoba 1963)[1] alikuwa mwimbaji nchini Ufaransa aliyependwa sana na wananchi. Jina lake la kuzaliwa ni Edith Giovanna Gassion lakini alichukua jina la kisanii "Piaf" (kifaransa kwa ndege shomoro). Wazazi walikuwa wahamiaji kutoka Italia, bibi yake upande wa mama alikuwa berberi kutoka Afrika Kaskazini. Wazazi hawakumtunza walimwachia kwa bibi upande wa baba na huyu alioongoza nyumba ya makahaba mjini Bernay (Normandie). Hapa alitunzwa na makahaba; kuna kumbkumbu ya kwamba alionjeka alipokuwa na miaka 5 akawa kipofu lakini makahaba wote walisimamisha kazi yao kwa siku tatu wakamwombea kanisani akaponyeka.

Alipokuwa na miaka 14 alichukuliwa na baba aliyejipatia maisha yake kwa kucheza mtaani mbele ya watu na hapa Edith alianza kuimba. Aliachana na baba akaedlea kujitegemea kama mwimbaji wa mtitaani. Kwa umri wa miaka 17 alipata mimba akamzaa binti aliyekufa baada ya miaka 2.

1935 alipokuwa na umri wa miaka 20 aliajiriwa mara ya kwanza na mwenye kilabu kwa programu ya kilabu chake. Hapa alikuwa maarufu haraka watu wengi walikuja kumsikia akarekodi diski zake za kwanza.

Baadaye alijulikana pia kitaifa. Marafiki walimsaidia kuandika nyimbo zilizolingana na maarafifa ya maisha yake na nyimbo hizi aligusa mioyo ya wananchi wengi. Baadaye alitunga nyimbo zake mwenyewe akapenda kusimulia hadithi kwa kuimba.

Kati ya nyimbo zale zilizopendwa haswa ni "La vie en rose" (1946), "Hymne à l'amour" (1949), "Milord" (1959) and "Non, je ne regrette rien" (1960).

Edith alikufa kwa umri wa miaka 47.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 11 Oktoba ni tarehe rasmi ya kifo chake; hali halisi aliaga dunia 10 Oktoba.