Ziwa Natron
| Ziwa Natron | |
|---|---|
| Nchi zinazopakana | Tanzania |
Ziwa Natron ni ziwa la chumvi lililopo kaskazini mwa Tanzania, karibu na mpaka wa Kenya, katika tawi la Afrika mashariki la Bonde la Ufa. Ziwa hili hulishwa na mto Ewaso Ng'iro na pia mito chemichemi zilizo tajiri kwa madini ambazo ni kina kabisa. Ziwa hili lina ukina wa chini ya mita tatu (fiti 10), na upana wake hutofautiana kwani hutegemea kiwango chake cha maji. Tofauti ya viwango vya maji kutokana na mabadiliko ya viwango vya uvukizi, ambavyo huacha viwango juu vya chumvi na madini mengine. Sehemu hii imezungukwa na eneo kavu na viwango vya mvua huyumbayumba. Mafukuto katika ziwa hili zaweza kufikia digrii 50 (celcius) au digrii 120 (Fahrenheit), na kutegemea mvua, alkalinity yaweza kufikia pH ya 9-10.5 (karibu kama vile alkali ya amonia).
Yaliyomo |
Flora [hariri]
Rangi ya ziwa hili ni tabia ya maziwa ambayo hupata viwango vya juu sana vya uvukizi. Maji inapovukiza wakati wa kiangazi, viwango vya chumvi huongezeka na kwa uhakika, vijinyama vipendao chumvi huanza kustawi. Baadhi ya vijinyama hivi nicyanobacteria, bakteria wadogo ambao hukua majini na hujitengenezea chakula kama mimea kupitia Usanisinuru (photosynthesis) . Pigmenti nyekundu ndani ya cyanobacteria hutoa kwa kirefu rangi nyekundu ya wazi wa maji ya ziwa, na rangi ya chungwa kwa sehemu kina ya ziwa. Chumvi ya alkali ambayo hukusanyika juu ya usawa wa ziwa, mara nyingi huwa na rangi nyekundu au pinki ambayo husababishwa na vijinyama vinavyopenda chumvi na ambavyo vinaishi huko. Vinamishi vya chumvi na sehemu zenye maji bichi karibu na pembe za ziwa kufanya mkono aina tofauti ya mimea.
Fauna [hariri]
Joto ya juu (hadi digrii 41 °C) na maudhui ya chumvi nyingi inayogeuka katika ziwa hili haifanyi mkono wanyamapori wengi. Hata hivyo ni makazi muhimu kwa aina ya ndege ya flamingo na pia ni makazi ya mwani, wanyama bila mifupa ya migongo na hata samaki ambao wanaweza kuishi katika maji ya chumvi. Hili ndilo ziwa pekee katika eneo la Afrika Mashariki ambalo kwa kawaida flamingo milioni 2.5 ambayo ni wadogo na ambayo huhofia maisha yao hufugwa . Kiwango ya chumvi kiongezekapo,cyanobacteria pia huongekeka, na ziwa yaweza kusaidia viota zaidi. Flamingo hawa, kundi kubwa zaidi katika Afrika Mashariki, hukusanyika pamoja katika maziwa ya chumvi, ambapo wao kujilisha Spirulina (mwani ya rangi ya buluu na kijani na pigmenti nyekundu). Ziwa Natron ni sehemu salama kufuga Flamingo wale wadogo kwa sababu mazingira yake ni kikwazo dhidi ya wanyama wanaokula wenzao wanaojaribu kufikia viota vyao. Flamingo wakuupia hufuga katika sehemu zenye ardhi zilizonyooka. Hata la kushangaza zaidi kuliko uwezo wa flamingo kuishi katika mazingira hayo ni kwamba spishi ya samaki, Tilapia wa alkali (Oreochromis alcalicus), hunawiri katika maji ya mito chemichemi.
Vitisho na Uhifadi [hariri]
Eneo linalozunguka ziwa hili la chumvi halijapangwa lakini kuna baadhi ya ufugaji na baadhi ya kilimo cha msimu. Vitisho kwa uwiano wa chumvi kutokana na ongezeko la maji bichi vitasababishwa na makadirio zaidi ya kukata magogo katika Natron na mtambo wa nguvu za umeme ya maji (hydroelectric power) iliyopangwa kuanzishwa katika Ziwa hili la Ewaso Ng'iro mpakani mwa nchi yaKenya. Ingawa mipango ya maendeleo ni pamoja na ujenzi wa lambo mwishoni mwa kaskazini mwa ziwa hili ili kushkilia maji safi, tishio la mchanganyiko katika ardhi hii bado ni mahututi. Hakuna ulinzi rasmi.
Tishio mpya kwa Ziwa Natron ni mapendekezo ya ukuzaji wa mtambo wa magadi katika mipaka yake. Mtambo huu utapampu maji kutoka kwa ziwa hili na kuchomoa sodium carbonate ambayo itabadilishwa kuwa poda ya kuosha ambayo hatimaye itasafirishwa. Kitachofuata mtambo huu kitakuwa makazi kwa zaidi ya wafanyakazi 1000 na kituo cha nguvu cha makaa chenye uwezo wa kutoa nishati kwa mtambo huu. Aidha, kuna uwezekano watengenezaji kuweza kuanzisha suriama ya uduvi wa maji ya chumvi kuongeza ufanisi wa uchimbaji.
Kulingana na Chris Magin, afisa wa kimataifa wa RSPB wa Afrika,nafasi ya flamingo wadogo kuendelea kufugwa katika uso wa uchinjanaji ni karibu sifuri. Maendeleo hii huenda yakapelekea flamingo wadogo kupotea katika Afrika Mashariki . Hivi sasa kundi lenye taasisi 20 za uhifadhi na mazingira kutoka Afrika Mashariki linaendesha kampeni duniani kote.Lengo kuu ni kusitisha mipango ya ujenzi wa kiwanda cha majivu ya magadi ambayo inafaa kujengwa na kampuni za Tata Chemicals Ltd ya Mumbai,India na National Development Corporation ya Tanzania. Kikundi hiki ambacho kinafanya kazi kutumia jina la Lake Natron Consultative Group linaratibiwa na Ken Mwathe, Mkuu wa Ikolojia wa African Conservation Centre.
Kwa sababu ya viumbe vyake hai vya vipekee, Tanzania iliitaja Bonde la Ziwa Natron katika Orodha ya Ramsar List of Wetlands of International Importance tarehe 4 Julai 2001. Ziwa hili pia ni eneo laWorld Wildlife Fund East African halophytics.
Kutembelea eneo [hariri]
Kuna idadi ya sehemu za kambi karibu na ziwa, ambayo pia ni msingi kwa ajili ya kupanda Ol Doinyo Lengai
Tazama pia [hariri]
Marejeleo [hariri]
- Lake Natron, Tanzania. Earth Observatory Newsroom. Rudishwa juu ya 2006-04-26.
- Lake Natron, Tanzania. Earth Observatory Newsroom. Rudishwa juu ya 2003-11-14.