Zaire (mkoa)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Zaire nchini Angola

Zaire ni jina la mkoa wa kaskazini-magharibi nchini Angola wenye eneo la km² 40,130 na wakazi 600,000.

Mipaka[hariri | hariri chanzo]

Mkoa umepakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo iliyoitwa "Zaire" hadi 1997. Mipaka mingine ni mikoa ya Uige upande wa mashariki, Cuanza Norte upande wa kusini na Bahari Atlantiki upande wa magharibi.

Miji[hariri | hariri chanzo]

Makako makuu ni mji wa M'banza-Kongo. Miji mingine ni Soyo kwenye mdomo wa mto Kongo, Tomboco, N'Zeto kwenye mdomo wa mto Mebridege na Noqui kando la Matadi kwenye mpaka wa Kongo.

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Uchumi ni hasa kilimo na uvuwi pamoja na migodi, kuchimba madini na mafuta ya petroli.


Makala hii kuhusu maeneo ya Angola bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Zaire (mkoa) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.