Yohane wa Dukla

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Yohane wa Dukla.

Yohane wa Dukla (kwa Kipolandi Jan z Dukly) alikuwa mtawa na padri wa shirika la Ndugu Wadogo kutoka Polandi[1]

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Yohane alizaliwa Dukla, Polandi, mwaka 1414 akafariki mwaka 1484 huko Lviv, leo nchini Ukraina.[2]

Ingawa alijiunga kwanza na Ndugu Wadogo Wakonventuali, baadaye akajiunga na urekebisho wa Observansya.

Hata baada ya kupofuka aliendelea kuandaa hotuba zake maarufu kwa kurudisha watu wengi kwenye Kanisa.[2]

Heshima baada ya kifo[hariri | hariri chanzo]

Mara baada ya kifo chake aliheshimiwa kama mtakatifu na miujiza mbalimbali ilisemekana kutokea kaburini pake.

Hatimaye, tarehe 10 Juni 1997, Papa Yohane Paulo II alimtangaza rasmi kuwa mtakatifu katika misa aliyoadhimisha huko Krosno, Poland, wakishiriki watu milioni 1 hivi.

Sikukuu yake ni tarehe 29 Septemba[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Patron Saints Index - Saint John of Dukla. Jalada kutoka ya awali juu ya 2011-12-31. Iliwekwa mnamo 2012-11-19.
  2. 2.0 2.1 Jones, p 273
  3. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Jones, Kathleen (2006). Butler's Lives of the Saints. New York: Continuum International Publishing Group. ISBN 0-86012-255-7. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.