Yohane wa Dameski

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Mt. Yohane wa Damasko.
Mt. Yohane wa Damasko

Yohane wa Dameski (kwa Kiarabu يوحنا ابن ﺳﺮﺟﻮﻥ Yuḥannā ibn Sarjūn) alikuwa mmonaki, padri na mwanateolojia kutoka Dameski mji mkuu wa Siria (676? - 749?).

Anaheshimiwa kama mtakatifu, babu wa Kanisa na mwalimu wa Kanisa. Ni msimamizi wa wachoraji.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 4 Desemba.

[hariri] Maisha

Alizaliwa katika familia ya Kiarabu ya Kikristo. Baba yake alikuwa Sarjūn ibn Manṣūr. Babu yake, Manṣūr, alikuwa wa kwanza katika familia kupewa vyeo vikubwa chini ya utawala wa halifa Mu'awiya bin Abi Sufyan na wa waandamizi wake.

Alipokuwa kijana alipata kuwa mshauri wa halifa wa Damasko na msimamizi wa mali.

Lakini baadaye akahukumiwa na kukatwa mkono wa kushoto. Hapo alihama mji huo na kujiunga na monasteri ya Mt. Saba, kati ya Bethlehemu na Yerusalemu, ambapo alifanya askofu.

Alihubiri na kuandika sana hadi kifo kilipompata akiwa na umri wa miaka 73.

Kitabu chake maarufu zaidi kinaitwa Kuhusu Imani Sahihi.

Alitumia nguvu zake zote hasa kutetea sanamu katika Ukristo. Alipewa ushindi na Mtaguso wa pili wa Nisea (787) baada ya kifo chake.

[hariri] Vyanzo

[hariri] Viungo vya nje

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine