Yobes Ondieki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Yobes Ondieki
Rekodi za medali
Men's Wanariadha
Anawakilisha nchi Bendera ya Kenya Kenya
World Championships
Dhahabu 1991 Tokyo 5000 m

Yobes Ondieki (mzaliwa 21 Februari 1961 katika katika wilaya ya Kisii, Nyanza) ni mwanariadha wa 5000m wa zamani wa Kenya aliyeshinda mashindano ya dunia mjini Tokyo 1991. Katika mwaka huohuo aliweka rekodi isiyokaa ya mita 5000 ya kenya ya dakika 13.02.82 huko mjini Zürich. Alishiriki katika fainali za Olimpiki za miaka ya 1988 na 1992 lakini hakushinda medali.

Ondieki alijulikana kwa zoezi zake ngumu na uwezo wake wa kukimbia daima kwa mwendo wa kasi. Hata hivyo, alikosa nguvu za kutosha za kumaliza, udhaifu uliotumiwa na wapinzani wake kumshinda katika Olimpiki ya mwaka 1992 katika fainali ya 5,000 m hukoBarcelona. (Baadhi yenu mtakumbuka kuwa mwaka wa 1992 ulikuwa mara ya kwanza na ya pekee ambapo mtu mweupe (Dieter Baumann) alishinda fainali za mita 5000 katika Olimpiki tangu Said Aouita kushinda mwaka 1984.) Mwaka 1993, Ondieki alikuwa mwanariadha wa kwanza kuvunja kizuizi cha dakika 27 akikimbia mita 10000 katika michezo ya Bislett huko Oslo.

Ondieki alifunga ndoa na Lisa Martin, mwanariadha wa Australia. Mwaka 1990 walikuwa na mtoto msichana aitwaye Emma Ondieki. Sasa hivi, Ondieki na Martin wameachana.

Mnamo Septemba 1991 yeye na Martin walihudhuria AFL Grand Final ya mwaka wa 1991 kama sehemu ya burudani kabla ya michezo.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Records
Alitanguliwa na
Kenya Richard Chelimo
Men's 10,000 m World Record Holder
10 Julai 1993 – 22 Julai 1994
Akafuatiwa na
Kenya William Sigei
Sporting positions
Alitanguliwa na
Kenya John Ngugi
Men's 5,000 m Best Year Performance
1989
Akafuatiwa na
Italia Salvatore Antibo
Alitanguliwa na
Italia Salvatore Antibo
Men's 5,000 m Best Year Performance
1991
Akafuatiwa na
Kenya Moses Kiptanui