William Edward Burghardt Du Bois
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
William Edward Burghardt Du Bois mwaka 1918
William Edward Burghardt Du Bois (alizaliwa Great Barrington, Massachusetts tar. 23 Februari 1868; aliaga dunia mjini Accra, Ghana tar. 27 Agosti 1963) alikuwa mwanahistoria, mtaalamu wa elimu ya jamii na mpigania wa haki za kibinadamu kutoka nchini Marekani. Alipigania hasa haki za watu weusi wenye asili ya Kiafrika.
Anakumbukwa kama mmoja kati ya mababa wa harakati ya Muungano wa Afrika.