Wilaya ya Mbulu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Mbulu (kijani cheusi) katika mkoa wa Manyara.

Wilaya ya Mbulu ni wilaya mojawapo kati ya 7 za Mkoa wa Manyara.

Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa Wilaya ya Mbulu ilihesabiwa kuwa 320,279 waishio humo. [1] Mwaka 2015 wilaya iligawiwa kwa Wilaya ya Mbulu Mjini na Wilaya ya Mbulu Vijijini. Katika sensa ya mwaka 2022 wazazi waliobaki upande wa vijijini walihesabiwa 238,272 [2].

Mbulu imepakana na Mkoa wa Arusha pamoja na ziwa Eyasi upande wa kaskazini, wilaya ya Babati upande wa mashariki, wilaya ya Hanang upande wa kusini na mkoa wa Singida kwa magharibi.

Wenyeji asilia ni hasa Wairaqw (Wambulu).

Makao makuu iko Mbulu mjini na mji huu ulianzishwa kama kituo cha Wamisionari wa Afrika wakati wa koloni la Afrika ya Mashariki ya Kijerumani kwa jina la Neu-Trier.

Mwaka 2018 iliamuliwa kujenga ofisi mpya kwa ajili ya Wilaya ya Mbulu Vijijini katika kata ya Haydom[3].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Sensa ya 2012, Manyara Region – Mbulu District-Council
  2. https://www.nbs.go.tz
  3. "Halmashauri ya Mbulu kuhamiwa Hydom", gazeti la Mwananchi, toleo la 28 Machi 2018, uk. 34
Kata za Wilaya ya Mbulu Vijijini - Mkoa wa Manyara - Tanzania

Bashay | Dinamu | Dongobesh | Endamilay | Eshkesh | Geterer | Gidhim | Haydarer | Haydom | Labay | Maghang | Maretadu | Masieda | Masqaroda | Tumati | Yaeda Ampa | Yaeda Chini


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Manyara bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Mbulu kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.