Wikipedia ya Kiswahili

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Favicon of Wikipedia Wikipedia ya Kiswahili
Wikipedia-logo-v2-sw.png
Kisara http://sw.wikipedia.org/
Ya kibiashara? Hapana
Aina ya tovuti Mradi wa Kamusi Elezo ya Interneti
Kujisajiri Hiari
Lugha asilia Kiswahili
Mmiliki Wikimedia Foundation
Ukurasa wa "Mwanzo" mwaka 2004

Wikipedia ya Kiswahili (au Wikipedia kwa Kiswahili) ni toleo la kamusi elezo ya Wikipedia kwa lugha ya Kiswahili. Wikipedia kwa Kiswahili ilianzishwa mnamo tar. 8 Machi katika mwaka wa 2003. Na kwa tar. 6 Machi, 2012, Wikipedia ya Kiswahili imefikisha makala zipatazo 23,292 na kuifanya iwe Wikipedia ya 80 kwa ukubwa.[1]

Katika Afrika, Wikipedia kwa Kiswahili ndiyo ya kwanza kwa ukubwahalafu inafuatiwa na Wikipedia ya Kiafrikaans. Na pia, kwa sasa ndiyo moja kati ya Wikipedia tatu tu za lugha za Niger-Kongo zenye makala zaidi ya 1,000 (na ndiyo ya kwanza kuvuka kiwango hicho), inafuata inakuwa Wikipedia ya Kiyoruba. Wikipedia kwa Kiswahili, ndiyo ya pili katika Afrika kuvuka kiasi cha makala 10,000 baada ya Wikipedia ya Kiafrikaans. [2] Mnamo tar. 20 Juni ya mwaka wa 2009, Wikipedia ya Kiswahili imebadilisha ukurasa wake wa mwanzo katika sura mpya.

Yaliyomo

[hariri] Maendeleo

Ilivyofika mnamo tar. 26 Septemba ya mwaka wa 2007, Wikipedia ya Kiswahili imefikisha makala 6,000. Mnamo tar. 21 Aprili ya mwaka wa 2008, Wikipedia ya Kiswahili imefikisha makala 7,000. Ilivyofika tar. 19 Desemba ya mwaka wa 2008, Wikipedia ya Kiswahili imefikisha makala 8,000, ni hasa baada ya kuanzishwa makala nyingi za mbegu za kata za Tanzania. Makala za mbegu ya Tanzania, ziliendelea kuisukuma Wikipedia ya Kiswahili hadi kufikia kiwango cha makala 9,000 na hiyo ilikuwa kunako tar. 2 Februari katika mwaka wa 2009. Mbegu ziliendelea hadi kufikia makala 10,000 (mnamo tar. 21 Februari ya mwaka 2009). Ilivyofikisha tar. 9 Aprili mwaka 2009, Wikipedia ya Kiswahili imefikisha kiwango cha makala 11,000. Kunako tar. 25 Aprili ya mwaka wa 2009, Wikipedia ya Kiswahili imefikisha makala 12,000. Mnamo mwezi wa Agosti ya tar. 17 katika mwaka wa 2009, Wikipedia ya Kiswahili imefikisha makala zipatazo 13,000, na kuendelea kuifanya iwe Wikipedia ya kwanza kwa ukubwa katika Afrika. Haikushia hapo na ilivyofika tar. 11 ya mwezi wa Septemba katika mwaka wa 2009, Wikipedia hii imefikisha makala 14,000.

[hariri] Tazama pia

[hariri] Marejeo

[hariri] Viungo vya Nje

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine