Wamaasai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Wamaasai, Kenya

Wamaasai ni kabila la watu wapatao 900,000 wanaoishi Kenya na Tanzania. Jina la jiji "Nairobi" limetokana na neno la Kimaasai Enkarenairobi (linalomaanisha "mahali penye maji baridi").

Kiasili Wamassai ni wafugaji wa ng'ombe lakini wengine wanafuga pia mbuzi, kondoo na ngamia. Mabadiliko ya maisha yameleta sehemu ya Wamassai kuishi mjini na pia kuanzisha kilimo cha mashamba.


WikiLettreMini.svg Makala hiyo kuhusu "Wamaasai" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Wamaasai kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.