Waidakho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Waidakho ni miongoni mwa makundi madogo ya kabila la Abaluhya wanaokalia eneo la rutuba nyingi la Kaunti ya Kakamega, Magharibi mwa Kenya. Eneo wanalokalia Waidakho linajulikana kiutawala kama Ikolomani, ambalo ndilo jimbo la uchaguzi pekee katika eneo hili, mji mkuu wake ukiwa Malinya. Mbunge wa sasa ni Bonny Khalwale.

Kama ilivyo na kawaida katika maeneo ya Kenya Magharibi, eneo la Idakho lina wingi wa wakazi huku makadirio ya idadi ya wakazi mwaka wa 2007 yakiwa yamezidi watu 150,000.

Upungufu wa mashamba na utandawazi vimewalazimu Waidakho kubadili mtindo wao wa maisha huku wengi wakijihusisha na ukulima wa ng'ombe wa maziwa na kwa kiwango kidogo, ukulima wa majani ya chai. Mhindi hata hivyo ndio mmea unaokuzwa zaidi, ukiwapa chakula chao cha kawaida - sima (ubushuma). Huvunwa mara mbili kwa mwaka.

Hata hivyo, hali yao ya kimaisha ya kiutamaduni huwasaidia tu kuishi maisha yao ya kisasa.

Wengi wao wakiwa na kiwango fulani cha masomo (62%), Waidakho siku hizi wanajiusisha kwenye sekta za biashara, wafanyakazi wa umma na sekta za binafsi kwenye miji mikuu ya Afrika Mashariki.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mwidakho pamoja na kaka yake, Mwisukha, wanaaminika kuwa waanzilishi wa makabila madogo ya Waidakho na Waisukha[1].

Makabila madogo ya Waidakho[hariri | hariri chanzo]

Abashimuli Abashikulu Abamasaba Abashiangala Abamusali Abangolori Abamahani [2]

Lugha[hariri | hariri chanzo]

Lugha ya Waidakho ni Kiidakho.

Dini[hariri | hariri chanzo]

Hakuna dini maalumu ya Waidakho. Hata hivyo, Ukristo ndio dini iliyoenea zaidi. Makweka -Friends- ndio maarufu. Madhehebu/makanisa mengine yaliyoko ni kama vile: Kanisa Katoliki, PAG na Legio Maria miongoni mwa mengine.

Sanaa na Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Fasihi[hariri | hariri chanzo]

Fasihi yao inajumuisha nyimbo na densi kiutamaduni. Kuna hata hivyo fasihi za kisasa kama vile tamthilia na riwaya ambazo pia wanahusikana nazo.

Vita vya Ng'ombe dume[hariri | hariri chanzo]

Licha ya kuwa mchezo wa kutumbuiza watu, pia ni sehemu ya mila zao ambapo hufanyika katika sherehe yoyote ya matanga na pia kwenye sherehe nyingine za kitamaduni. Mchezo huu huusisha ng'ombe dume na hufanyika mathalani asubuhi na mapema.

Densi ya Isukuti[hariri | hariri chanzo]

Isukuti ni aina ya ngoma iliyoundwa kutoka kwa ngozi maalumu. Densi ya Isukuti ni maarufu miongoni mwa jamii ya Abaluhya, Waidakho wakiwemo. Densi hii huchezwa katika sherehe za kitamaduni kama vile matanga na harusi. Pia densi hii hutumika kusherehekea hasawa katika michezo kama vile kandanda. Mashabiki wa AFC Leopards, timu ambayo inajumuisha Waluhya na iliyoanzishwa kwa misingi ya Uluhya, hucheza Isukuti kwa kushangilia timu yao katika mechi za Ligi Kuu ya Kenya.

Lipala[hariri | hariri chanzo]

Lipala ni mtindo wa kucheza miongoni mwa jamii za Waluhya. Mtindo huu hujumuisha mchezaji kupiga makofi na kisha kushika kichwa chake na mkono mmoja huku mkono mwingine ukiwa kwenye kiuno huku akikitisa.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2010-04-28. Iliwekwa mnamo 2010-04-06. 
  2. Lennox Ludenyo Amalemba


Makala hii kuhusu utamaduni wa Kenya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Waidakho kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.