Volta ya Juu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Volta ya Juu
Ramani ambayo inaonyesha mikono ya mto Volta nchini

Volta ya Juu (kwa Kifaransa: Haute Volta) lilikuwa jina la koloni la Kifaransa na tangu mwaka 1960 nchi huru ya Afrika ya Magharibi inayoitwa Burkina Faso tangu mwaka 1984.

Jina limetokana na mto Volta unaoanzia hapa.

Nchi ilianzishwa kwa njia ya kugawa koloni la Cote d'Ivoire mwaka 1919.

Kati ya miaka 1932 na 1947 eneo lake lilitawaliwa na makoloni ya jirani.

Kiongozi wa nchi Thomas Sankara alibadilisha jina la nchi tarehe 4 Agosti 1984.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Volta ya Juu kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.