Volta (mto)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mto wa Volta
Mto Volta kusini ya lambo la Akosombo
Chanzo maungano ya mito ya Muhun, Nazinon na Nakambe karibu na mji wa Salaga (Ghana)
Mdomo Bahari ya Atlantiki
Nchi Ghana
Urefu 2,574 km pamoja na tawimto wa Muhun (Volta Nyeusi)
Kimo cha chanzo 180 m kwenye maungano ya mito
Matawimto ya Volta ndiyo Muhun (Volta nyeusi), Nazinon (Volta nyekundu) na Nakambe (Volta nyeupe) pamoja na maungano ya mito katika Burkina Faso na Ghana.

Volta ni mto muhimu wa Afrika ya Magharibi. Inaanza katika maungano ya matawimto yake ya Muhun (Volta nyeusi), Nazinon (Volta nyekundu) na Nakambe (Volta nyeupe) karibu na mji wa Salaga, Ghana.

Katika Ghana boma la lambo la Akosombo (Ghana) limesababisha kutokea kwa ziwa Volta ambalo ni lambo kubwa kabisa duniani. Baada ya kuondoka katika ziwa hilo lisilo asilia Volta inaingia katika Ghuba ya Guinea ya bahari Atlantiki.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Volta (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.