Vinsenti Pallotti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ya Mt. Vinsenti Pallotti.

Vinsenti Pallotti (Roma, Italia, 21 Aprili 1795 – Roma, 22 Januari 1850) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mwanzilishi wa Shirika la Utume Katoliki.

Kwa maandishi yake na kwa miundo ya namna hiyo aliyoianzisha alichochea wito wa Wakristo wote wa kulifanyia Kanisa kazi kwa bidii.

Alitangazwa na Papa Pius XII kuwa mwenye heri tarehe 22 Januari 1950, halafu mtakatifu na Papa Yohane XXIII tarehe 20 Januari 1963.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 22 Januari[1].

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.