Victoria (ziwa)
| Ziwa la Viktoria Nyanza | |
|---|---|
|
|
|
| Mahali | Afrika ya Mashariki |
| Nchi zinazopakana | Tanzania, Kenya na Uganda |
| Eneo la maji | 68,100 km² |
| Kina ya chini | 81 m |
| Mito inayoingia | Kagera, Katonga, Nzoia |
| Mito inayotoka | Nile |
| Kimo cha uwiano wa maji juu ya UB | 1,134 m |
| Miji mikubwa ufukoni | Kampala, Kisumu, Mwanza |
Ziwa Victoria (pia: Viktoria Nyanza, Ziwa Nyanza) ni ziwa kubwa kuliko yote barani Afrika, na la pili duniani. Ziwa la kwanza ni Ziwa Superior ambalo lipo Amerika ya Kaskazini.
Ziwa Victoria lipo mita 1134 juu ya usawa wa bahari na lina eneo la kilometa za mraba zaidi ya 68,100.
Maji ya ziwa Victoria yanamiminika kwenye mto Nile na kuelekea bahari ya Mediteranea kwa umbali wa maili 4,000.
Ziwa Victoria limekuwa ni kiunganisho na mpaka kwa nchi tatu za Afrika ya mashariki ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda.
Ziwa hili linapata maji yake mengi kutokana na mvua (80%) na kutoka vijito vingi vidogo. Mto mkubwa unaoingia Victoria ni Mto Kagera unaotiririka kutoka upande wa magharibi.
Ziwa hili lina kina cha wastani cha mita 40 (futi 130) na mwambao wa urefu wa mita 4,828 (maili 3,000), visiwa vyake vikiwa vimechangia 3.7% ya urefu huu. Eneo la maji ya ziwa imegawanywa 6% (4,100 km2) nchini Kenya, 45% (31,000 km2) nchini Uganda, na 49% (33,700 km2) nchini Tanzania.
Viungo vya Nje [hariri]
Watersheds of Africa: A10 Nile | Lake Victoria
| Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Victoria (ziwa) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |