Urekebisho wa Kikatoliki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Undani wa Chiesa del Gesù, mjini Roma, kielelezo cha Urekebisho wa Kikatoliki. Humo amezikwa Ignas wa Loyola, mwanzilishi wa Wajesuiti, shirika la kitawa muhimu zaidi katika kupinga uenezi wa Uprotestanti.

Urekebisho wa Kikatoliki ulikuwa kipaumbele cha Wakristo wengi wa Kanisa Katoliki hasa katika karne XV na XVI.

Juhudi hizo zilikuwa na upana mkubwa na kuhusu kwa namna ya pekee mambo matano yafuatayo:

  1. Mafundisho ya imani
  2. Miundo ya Kanisa
  3. Utawa
  4. Matapo ya kiroho
  5. Majukumu ya kisiasa

Juhudi hizo zilipata nguvu mpya baada ya Matengenezo ya Kiprotestanti (yaliyoanzishwa na Martin Luther mwaka 1517) kupamba Ulaya Kaskazini kuanzia Ujerumani. Kwa sababu hiyo ukaja kuitwa (1776) 'Counter-Reformation'. Ukweli ni kwamba urekebisho wa Kikatoliki ulianza kabla ya Uprotestanti, hasa Italia, ukaendelea sambamba nao.

Pamoja na hayo ni kwamba, baada ya Uprotestanti kuanza, juhudi zilielekea pia kuzuia uenezi wake na kuurudisha nyuma katika maeneo mbalimbali, k.mf. Polandi.

Kikao cha Mtaguso wa Trento kilivyochorwa wakati huo

Juhudi hizo zilipitishwa na Mtaguso wa Trento, ambao ndio mtaguso mkuu wa Kanisa Katoliki uliodumu muda mrefu zaidi (15451563) na kutoa mafundisho na maagizo mengi zaidi.

Katika hayo upande mmoja ilionekana nia ya kupokea baadhi ya hoja za Waprotestanti, ambao kwa wakati huo walikuwa wameshagawanyika makundimakundi, upande mwingine ilionekana nia ya kutetea imani sahihi ya mapokeo ya mitume pale ambapo msimamo wa Waprotestanti ulitazamwa kuwa uzushi, kwa mfano kuhusu sakramenti.

Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Urekebisho wa Kikatoliki kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.