Uhaini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uhaini (kutoka neno la Kiarabu) ni pale mtu anapotenda jambo dhidi ya nchi yake. Kwa mfano, mtu anaweza kuisaidia nchi nyingine ipigane vita dhidi ya nchi yake kwa kutoa habari za siri.

Uhaini ni neno la kawaida, lakini nchi tofauti zina sheria na adhabu tofauti dhidi ya matendo ya kihaini, hata adhabu ya kifo.

Miongoni mwa wahaini maarufu duniani kuna Yuda Iskarioti, Benedict Arnold, Philippe Pétain na Vidkun Quisling.

Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uhaini kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.