Ubangi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ubangi (mto))
Mto wa Ubangi
Ubangi inavyoonekana kutoka angani kati ya maeneo ya mashamba na msitu wa mvua
Chanzo Maungano ya mito Mbomou na Uele mpakani wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mdomo Mto Kongo (karibu na Mbandaka)
Nchi Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kongo
Urefu 850 km, pamoja na Uele 2.272 km
Tawimito Mbomou, Uele
Mkondo 7,000 m³/s
Eneo la beseni 613,202 km²
Miji mikubwa kando lake Bangui

Ubangi ni tawimto mkubwa wa mto Kongo na kati ya mito mirefu ya Afrika.

Chanzo chake ni maungano ya mito Mbomou na Uele kwenye mpaka wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (J.A.K.) na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (J.K.K.).

Mto waelekea kwanza magharibi halafu magharibi-kusini ukipitia mji mkuu Bangui.

Mwendo wote wa mto Ubangi ni mpaka wa kimataifa: kwanza kati ya J.A.K. na J.K.K., halafu kati ya J.K.K. na Jamhuri ya Kongo.

Ubangi waishia katika mto Kongo takriban kilomita 90 kusini kwa mji wa Mbandaka.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ubangi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.