Turibio wa Mongrovejo
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu Turibio wa Mongrovejo (16 Novemba 1538 – 23 Machi 1606) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki nchini Peru.
Ametambuliwa kuwa mtakatifu. Tarehe ya kifo chake, yaani 23 Machi pia ni sikukuu yake.
Maisha [hariri]
Turibio wa Mongrovejo alizaliwa nchini Hispania mnamo mwaka 1538.
Alijifunza sheria huko Salamanka, na mwaka 1580 aliteuliwa kuwa Askofu wa Lima nchini Peru, akaenda Amerika.
Alikuwa motomoto kwa kazi za kitume, akiitisha mikutano mbalimbali ili kurekebisha mambo ya dini katika nchi nzima.
Kwa nguvu zote alitetea haki za Kanisa, aliwatembelea Wakristo waliokuwa chini yake, na kufanya kazi kwa muda mrefu kwa mafaa ya wenyeji wa Peru.
Alikufa mwaka 1606.
Tazama pia [hariri]
Viungo vya nje [hariri]
- "St. Toribio Alfonso Mogrovejo". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913. http://www.newadvent.org/cathen/14781a.htm.
- TURIBIUS of Mogroveio
- His biography at Lives of the Saints
- (Kihispania) Short biography at MSN Encarta
- [1]
| Makala hii kuhusu Mkristo huyu bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Turibio wa Mongrovejo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |