Tumbusi
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Tumbusi | ||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
|
Tumbusi au tai mzoga ni ndege wakubwa katika familia Accipitridae ambao hula mizoga. Wana mnasaba na tai. Huko Amerika kuna ndege wafananao na tumbusi, lakini wale hawana mnasaba sana na huwekwa katika familia Cathartidae. Tumbusi huvumbua mizoga kwa macho, lakini wale wa Marekani wananusa vizuri pia.
Spishi nyingi za tumbusi zina kichwa bila manyoya. Sifa bainifu hii imekua kuzuia manyoya ya kichwa yasichafuliwe kwa damu wakati tumbusi akiingiza kichwa chake ndani ya mzoga. Kichwa wenye upara kinaweza kusafishwa kwa urahisi ndani ya mto au ziwa.
[hariri] Spishi za Afrika
- Aegypius monachus, Tumbusi Mweusi (Eurasian Black Vulture or Monk Vulture)
- Gypaetus barbatus, Tumbusi Mlakondoo (Lammergeier or Bearded Vulture)
- Gypohierax angolensis, Tumbusi-miwese (Palm-nut Vulture)
- Gyps africanus, Tumbusi Mgongo-mweupe (White-backed Vulture)
- Gyps coprotheres, Tumbusi Kusi (Cape Vulture)
- Gyps fulvus, Tumbusi wa Ulaya (Eurasian Griffon Vulture)
- Gyps rueppellii, Tumbusi-mbuga (Rüppell's Griffon Vulture)
- Necrosyrtes monachus, Tumbusi Kapuchini (Hooded Vulture)
- Neophron percnopterus, Tumbusi Uso-njano (Egyptian Vulture)
- Torgos tracheliotus, Tumbusi Ngusha (Nubian or Lappet-faced Vulture)
- Trigonoceps occipitalis, Tumbusi Kichwa-cheupe (White-headed Vulture)
[hariri] Spishi za mabara mengine
- Gyps bengalensis (Indian White-rumped Vulture)
- Gyps indicus (Indian Vulture)
- Gyps himalayensis (Himalayan Griffon Vulture)
- Gyps tenuirostris (Slender-billed Vulture)
- Sarcogyps calvus (Red-headed Vulture)