Tumbusi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tumbusi
Tumbusi uso-njano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Accipitriformes (Ndege kama vipanga)
Familia: Accipitridae (Ndege walio na mnasaba na vipanga)
Vieillot, 1816
Ngazi za chini

Nusufamilia 2, jenasi 9 za tumbusi:

Tumbusi au tai mzoga ni ndege wakubwa wa nusufamilia Aegypiinae na Gypaetinae katika familia Accipitridae ambao hula mizoga. Wana mnasaba na tai. Huko Amerika kuna ndege wafananao na tumbusi, lakini wale hawana mnasaba sana na huwekwa katika familia Cathartidae. Tumbusi huvumbua mizoga kwa macho, lakini wale wa Marekani wananusa vizuri pia.

Spishi nyingi za tumbusi zina kichwa bila manyoya. Sifa bainifu hii imekua kuzuia manyoya ya kichwa yasichafuliwe kwa damu wakati tumbusi akiingiza kichwa chake ndani ya mzoga. Kichwa chenye upara kinaweza kusafishwa kwa urahisi ndani ya mto au ziwa.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]