Tuesday Kihangala

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Faili:Harusi ya Candy.jpg
Moja kati ya Filamu alizoongoza Kihangala ni hii

Tuesday Kihangala (amezaliwa tar. 14 Novemba 1971) ni mwongozaji na mtunzi wa filamu kutoka nchini Tanzania. Aliwahi kuigiza kidogo sana katika kundi la sanaa la Kaole, na baadaye kwenda kujianzishia kundi lake mwenyewe la maigizo ya sanaa nchini Tanzania. Kundi linakwenda kwa jina la "Fukuto" lenye makazi yake huko Kinondoni jijini Dar es Salaam, Tanzania. Hivi karibuni wanatamba na tamthilia ya Jumba la Dhahabu, inayoonyeshwa na Televisheni ya Taifa ya Tanzania.

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tuesday Kihangala kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.