Thika (mto)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mto Thika

Mto Thika unapatikana katika kaunti ya Kiambu katikati ya Kenya.

Ni tawimto la mto Tana ambao ndio mrefu kuliko yote nchini na unaishia katika Bahari ya Hindi.

Mto Thika ni chanzo cha nishati ya maji, na pia hutoa maji kwa Nairobi, mji mkuu wa Kenya.

Jina la Thika halijulikani kama limetoka lugha ya Kikuyu ama lugha ya Kimaasai. Katika Kikuyu, guthika maana yake kuzika; na katika Kimaasai, jina linafanana na sika maana yake kusugua ukingoni.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]