Theodosius Mkuu
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Theodosius I)
Flavius Theodosius (11 Januari, 347 – 17 Januari, 395) alikuwa Kaizari wa Dola la Roma kuanzia 15 Mei, 392 hadi kifo chake. Kabla hajatawala dola zima, alikuwa Kaizari upande wa Mashariki kuanzia Agosti 378. Upande wa Mashariki alimfuata Valens. Theodosius alikuwa Kaizari wa mwisho aliyetawala dola zima la Roma. Wana wake wawili walishiriki utawala, Honorius upande wa Magharibi, na Arcadius upande wa Mashariki.
| Makala hii kuhusu Kaizari fulani wa Roma bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Theodosius Mkuu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |