Terror Squad

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kwa matumizi mengine ya Terror Squad, angalia Terror Squad (maana)

Terror Squad
Logo yao
Logo yao
Maelezo ya awali
Asili yake The Bronx, New York
Aina ya muziki Gangsta rap
Latino rap
Hardcore rap
East Coast Rap
Miaka ya kazi 1999 - hadi leo
Studio Koch Records
Terror Squad Entertainment
Wanachama wa sasa
Fat Joe
Pistol Pete
Cool & Dre
Kill All Rats Mafia
O.Z.
H Mob
The Leader
Nu Jerzey Devil
Wanachama wa zamani
DJ Khaled
Big Pun
Cuban Link
Triple Seis
Prospect
Tony Sunshine
Remy Ma
Armageddon

Terror Squad ni kundi la muziki wa hip hop na pia studio kutoka mjini Bronx, New York, ambalo lilianzishwa mnamo mwaka 1998 kwa kupitia kibao kimoja mashuhuri kinachotoka katika albamu ya Don Cartagena ya mwimbaji kiongozi wa kundi hilo Fat Joe.[1]

Walitoa albamu yao ya kwanza iliyojulikana kwa jina la Terror Squad, kunako 1999, ikiwa imeambatana na kibao chao cha kwanza kilichokwenda kwa jina la "Whatcha Gon' Do", ambacho kiliimbwa zaidi na Big Punisher, ambaye alifariki dunia kwa tatizo la ugonjwa moyo manmo mwa 2000. Baada ya kifo cha Big Pun, washikaji zake wa toka kitambo Bw. Cuban Link na Triple Seis, wakajitoa katika kundi na badala yao nafasi hizo zikawa nimeshikiliwa na Remy Martin na Tony Sunshine.

Kama jinsi vile kundi lilivyo simama kwa kufuatia kifo cha Big Pun, wanachama wengi wa kundi hilo wakaangukia katika fumbo zito kwa kufuatia mafanikio makubwa alioyoyapata rapa mwenzao Fat Joe, akiwa kama msanii wa kujitegea na kuwashinda hata wale wenzake.

Kundi lilirudi tena ulingoni na wakafanikiwa kutoa albamu yao ya pili iliyokwenda kwa jina la True Story, mnamo mwaka wa 2004. Albamu ilibeba byimbo maarufu ya "Lean Back," ambayo ilitayarishwa na Scott Storch, na kuweza kushika nafasi ya kwanza katika chati za Billboard Hot 100 bora na nafasi ya 24 katika UK.[2]

Muziki[hariri | hariri chanzo]

Album[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]