Teofilo wa Corte

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake katika kanisa la Alando.

Teofilo wa Corte (Corte, Corsica, leo nchini Ufaransa, 30 Oktoba 1676 - Fucecchio, leo nchini Italia, 19 Mei 1740), mwanafunzi wa Thomas wa Cori, alikuwa padri wa shirika la Ndugu Wadogo na mhubiri maarufu.

Jina lake la awali lilikuwa Biagio Arrighi. Alijulikana kwa heshima yake kubwa kwa Mateso ya Yesu na kwa Bikira Maria.

Alijitahidi kueneza urekebisho shirikani kwa kuanzisha mahali pa upwekeni[1].

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu tangu tarehe 29 Juni 1930, alipotangazwa na Papa Pius XI.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/54000
  2. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.