Sululu-uzuri (au Sururu-uzuri) ni ndege wa jenasiRostratula na Nycticryptes katika familiaRostratulidae. Wakifanana na sululu, kwa kweli wana mnasaba zaidi na sile-maua. Wana rangi kali kuliko sululu na jike, kama yule wa sile-maua, ni mkubwa na ana rangi kali zaidi kuliko dume ambaye huatamia mayai na kutunza makinda. Wanatokea katika vinamasi na mabwawa ya matete na hutembea wakati wa utusitusi na mwanzo wa usiku. Hula mbegu, wadudu, gegereka, makoa na nyungunyungu. Jike hutaga mayai 2-4 ndani ya tundu juu ya biwi la mimea.