Sikonge

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Kata ya Sikonge
Nchi Tanzania
Mkoa Tabora
Wilaya Sikonge
Idadi ya wakazi
 - Mji 24,917

Sikonge ni makao makuu ya wilaya ya Sikonge katika Mkoa wa Tabora nchini Tanzania.

Kufuatana na sensa ya mwaka 2002 Sikonge ilikuwa na wakazi 24,917 [1]

Sikonge kama mji umegawanyika katika sehemu kuu mbili, Misheni na Madukani. Upande wa misheni ni sehemu walipojenga Wakristo wa Moravian kanisa lao na misheni yao yaani shule, hospitali na chuo cha uuguzi. Shule yao ya sekondari iko upande wa Madukani. Hamna mgawanyiko maalumu wa Wakristo na Waislam.

Ila Madukani ni sehemu wanapokaa Waarabu wengi na maduka yao na hiyo imepelekea sehemu hiyo iitwe hivyo. Upande huo pia kuna Mahakama, benki, kanisa la Wakatholiki Warumi (Roman Catholic Church) na shule ya sekondari Mbirani. Hii shule ni shule ya siku nyingi sana na enzi hizo ilikuwa ikiitwa Middle School na hivyo wasomi wengi kutoka Sikonge utakuta walisoma hapa. Baadaye ilitaifishwa na kuwa shule ya msingi na si miaka mingi sana ilirudishwa kwa Wamoravian na wakaifanya kuwa shule ya Sekondari. Serikali ilijenga shule nyingine mpya na shule hiyo ikachukua jina hilo hilo na Mbirani na huku sekondari ikiitwa Sikonge Secondary School.

Marejeo ya Nje [hariri]

  1. http://www.tanzania.go.tz/census/census/districts/sikonge.htm Sensa ya 2002 kwa Sikonge
Flag-map of Tanzania.svg Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Tabora bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Sikonge kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.