Tezi (meli)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Shetri)

Kwa kundinyota linaloitwa Shetri tazama hapa Shetri (kundinyota)

Tezi ya jahazi ya kihistoria

Tezi (au: shetri) ni sehemu ya nyuma ya meli. Huko kuna usukani wa chombo unaoelekeza meli kule inakotakiwa kuelekea. Ni pia mahali pa rafadha inayosukuma chombo mbele.

Kwa meli kubwa za uvuvi mara nyingi nyavu za kunasia samaki huteremshwa tezini.