Shahada
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Shahada kwenye bendera ya Uarabuni wa Saudia
Shahada ni ungamo wa imani ya Kiislamu.
Tamko hili lina maneno yafuatayo: لا إله إلا الله محمد رسول الله (Kiarabu: Lā ilāhā illā-llāhu; muhammadun rasūlu-llāhi). Maana yake ni: "Hakuna mungu ila Allah; Muhammad ni mtume wa Allah". Katika sala maneno haya huanzishwa kwa "أشهد أن" (yaani: Nakiri kwamba...).
Kwa maneno haya Mwislamu hutamka kuwa
- Mungu (Allah) ni mmoja tu hakuna mwingine
- Muhammad ni mtume na rasul wake wa mwisho.
Shahada ni moja ya nguzo tano za Uislamu. Hurudiwa kila siku na Mwislamu akifuata wajibu wake wa sala.
Kuna Washia kadhaa wanaoongeza maneno "Alīyun wali Allah" (علي ولي الله - "Ali rafiki yake Mungu") wakitaka kukiri ya kwamba katika imani yao Ali ni kiongozi teule wa Waislamu.
Kutamka shahada kwa imani ni tendo la kujiunga na Uislamu na kuwa Mwislamu.

