Samweli
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ndogo inayomchora Samweli akimweka wakfu mfalme Daudi
Samweli (kwa Kiebrania: שְׁמוּאֵל Šəmuʼel, maana yake labda ni "Anayemsikiliza Mungu") ni mtu muhimu wa Historia ya wokovu ya Agano la Kale.
Katika Biblia anatajwa kama mwamuzi na kama nabii, naye ndiye mwanzilishi wa ufalme wa Israeli.
Habari zake zinasimuliwa katika Vitabu vya Samweli.
Kanisa Katoliki linamheshimu kama mtakatifu hasa tarehe 20 Agosti.