Saddam Hussein

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Saddam Hussein

Saddam Hussein Abd al-Majid al-Tikriti (28 Aprili 1937 - 30 Desemba 2006) alikuwa Rais wa Iraki, kuanzia tarehe 16 Julai 1979 hadi mwaka wa 2003, pia waziri mkuu wa Iraki kati ya 1994 na 2003.

Alipanda ngazi ndani ya serikali na chama cha Baath kama makamu wa rais aliyemtangulia Ahmad Hasan al-Bakr. Baada ya kupewa cheo cha rais aliua wapinzani wengi na kuimarisha utawala wake.

Akaanzisha vita mbili:

Ndani ya Iraki alipigania upinzani wa sehemu kubwa za wananchi hasa katika kampeni dhidi ya Wakurdi kaskazini mwa Iraki wakati wa vita dhidi ya Uajemi na dhidi ya Washia wa Iraki Kusini baada ya vita ya Ghuba.

Saddam Hussein aliondolewa madarakani wakati wa uvamizi wa Iraki na Marekani katika vita ya pili ya ghuba mwaka 2003. Alienda mafichoni kwa miezi kadhaa, akakamatwa na kupelekwa mbele ya mahakama ya Kiiraki iliyompa adhabu ya kifo kwa jinai dhidi ya binadamu na hasa kesi 148 za mauaji zilizothibitishwa mahakamani.

Alinyongwa Desemba 2006 katika kambi la kijeshi mjini Al Kadhimiya nchini Iraki.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Saddam Hussein kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  1. [1] Archived 8 Agosti 2008 at the Wayback Machine.[2]