Safu ya Ruwenzori

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ruwenzori)
Safu ya Rwenzori kusini kwa Fort Portal (Uganda).
Mimea ya pekee ya Rwenzori.

Safu ya Ruwenzori (pia: Rwenzori) ni eneo la milima katika Afrika ya Kati kwenye mpaka wa Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mlima wa juu ni Pic Marguerite (Mlima Stanley) wenye kimo cha mita 5,109 juu ya UB. Mingine ni mlima Speke (m 4,890), mlima Baker (m 4,844), mlima Emin (m 4,798), mlima Gessi (m 4,715) na mlima Luigi di Savoia (m 4,627).

Baada ya Kilimanjaro na mlima Kenya, Ruwenzori ni mlima mkubwa wa tatu barani Afrika. Pamoja na hiyo miwili ndiyo milima pekee yenye barafuto za kudumu kwenye bara hilo.

Huaminiwa ya kwamba Rwenzori ni ile "Milima ya Mwezi" iliyotajwa katika taarifa za Klaudio Ptolemaio zamani za Misri ya Kale.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Safu ya Ruwenzori kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.