Rupia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Robo rupie ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani ("Deutsch Ostafrika")

Rupia ni jina la pesa inayotumika leo huko India na katika nchi mbalimbali za Asia.

Ni pia jina la pesa iliyowahi kutumika Afrika ya Mashariki na nchi mbalimbali.

Jina na historia[hariri | hariri chanzo]

Rupia (1887) Uhindi ya Kiingereza, Victoria

Neno "rupia" limetokana na lugha ya Kihindi cha kale "rūp" au "rūpā" linalomaanisha "fedha". Katika lugha ya Sanskrit "rupyakam" (रूप्यकम्) inamaanisha sarafu ya fedha. Hii ni asili ya "Rūpaya" iliyotumika katika India kama sarafu yenye gramu 11.66 za fedha tangu mwaka 1540. Rupia moja ilikuwa na Anna 16, Paisa 64 au Pai 192.

Pesa ya kisasa[hariri | hariri chanzo]

Leo hii nchi zifuatazo zinatumia jina la Rupia (Rupiah, Rupee: ₨) kwa pesa zao:

Pesa ya kihistoria[hariri | hariri chanzo]

Rupia ilikuwa pesa ya nchi na maeneo yafuatayo:

Picha[hariri | hariri chanzo]