Rosa wa Viterbo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rosa wa Viterbo akishika msalaba na kuwa na mawaridi, kutokana na jina lake (Rosa=Waridi).

Rosa wa Viterbo (Viterbo, leo mkoani Lazio, Italia, 1233 hivi – 6 Machi 1251[1] ) alikuwa msichana maarufu kwa imani yake katika Ukristo aliyejiunga mapema sana na Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisko.

Baada ya kuishi kama mkaapweke kuanzia umri wa miaka 7, alianza kuhubiri toba na upatanisho hata alipofukuzwa mjini (1250).

Mwaka huohuo, baada ya Papa kuteka tena Viterbo, alirudishwa kutokana na karama zake za uponyaji na unabii, lakini akafariki mapema kutokana na afya yake mbovu toka zamani.

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mwenye heri bikira.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Machi[2] au 4 Septemba, siku ambapo maiti wake asiyeoza ardhini alihamishiwa kanisani (1258). Mpaka leo moyo wake ni mzima.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Cleary, Gregory. "St. Rose of Viterbo." The Catholic Encyclopedia. Vol. 13. New York: Robert Appleton Company, 1912. 5 Mar. 2013
  2. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • De Kerval, Ste Rose, sa vie et son temps (Vanves, 1896);
  • Pizzi, Storia della Città di Viterbo (Rome, 1887).

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.