Rosa wa Lima

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Rosa wa Lima
alivyochorwa na Claudio Coello (16421693), Prado, Madrid, Hispania.

Rosa wa Lima ni jina lililoenea la Isabel Flores y de Oliva (20 Aprili 158624 Agosti 1617), binti wa Wahispania waliohamia Lima, Peru.

Alipata umaarufu kwa juhudi zake katika maisha ya kiroho na kwa huduma zake za huruma kwa maskini wa mji wake huo.

Mlei wa Utawa wa Tatu wa Mt. Dominiko na bikira, ni Mwamerika wa kwanza kutangazwa mtakatifu katika Kanisa Katoliki. Kwanza alitangazwa mwenye heri na Papa Klementi IX tarehe 10 Mei 1667, halafu mtakatifu tarehe 12 Aprili 1671 na Papa Klementi X.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 23 Agosti[1]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Teodoro Hampe Martínez. "Santa Rosa de Lima y la identidad criolla en el Perú colonial" (essay of interpretation), Revista de Historia de América, No. 121 (January – December, 1996), pp. 7–26

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.