Romualdo Abati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Romwald abati)
Mchoro wa Guercino, San Romualdo, Ravenna.

Mtakatifu Romualdo (Ravenna, Emilia-Romagna, 951 / 953 - karibu na Fabriano, Marche, 19 Juni 1027) alikuwa abati nchini Italia na mwanzilishi wa urekebisho wa Wabenedikto Wakamaldoli.

Anaheshimiwa kama mtakatifu na Kanisa Katoliki kuanzia miaka 5 baada ya kufa, na hasa tangu mwaka 1595.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 19 Juni[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Maisha yake yamesimuliwa na mfuasi wake Petro Damiani katika kitabu alichokiandika miaka 15 hivi baada ya kifo chake (1042).

Kitabu rasmi cha watakatifu wa Kanisa la Roma (Martirologium Romanum) kinamkumbuka hivi: "Mtakatifu Romualdo, mkaapweke na baba wa wamonaki Wakamaldoli, ambaye, akiwa na asili ya Ravenna, na kutamani kushika maisha na nidhamu ya wakaapweke, alizunguka Italia miaka mingi, akijenga monasteri ndogo na kuhimiza kokote wamonaki wafuate maisha ya Kiinjili, mpaka alipomaliza vizuri juhudi zake katika monasteri ya Val di Castro mkoani Marche" [2].

Sala yake[hariri | hariri chanzo]

Yesu mpenzi, amani ya moyo wangu, hamu isiyosemeka, utamu na unono wa malaika na wa watakatifu!

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.