Rahabu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro wa James Tissot, Kahaba wa Yeriko na Wapelelezi Wawili.

Rahabu (kwa Kiebrania רָחָב Raẖav au Rāḥāḇ, maana yake "mpana") alikuwa mwanamke wa Yeriko wakati ambapo Waisraeli, wakiongozwa na Yoshua, walivamia nchi ya Kanaani katika karne ya 13 KK.

Kitabu cha Yoshua (2:1-7) kinasimulia jinsi huyo kahaba alivyokaribisha wapelelezi wawili wa Israeli, alivyowaficha wasikamatwe na wenyeji, na alivyowadai wamuapie watamuokoa pamoja na familia yake Mungu atakawapowajalia kuteka mji huo.

Ingawa Rahabu alifanya kazi haramu akasaliti mji wake, anasifiwa na Barua kwa Waebrania (11:31) kwa imani yake iliyomuokoa na kumuingiza katika taifa la Mungu. Pia anasifiwa na Barua ya Yakobo (2:25) kama kielelezo cha mtu anayetenda mema.

Rahabu (kwa Kigiriki Ῥαχάβ, Rakhab) anatajwa na Injili ya Mathayo (1:5) katika kitabu cha ukoo cha Yesu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]