Papa Leo IX

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Pope Leo IX)
Mt. Leo IX.

Papa Leo IX (21 Juni 100219 Aprili 1054) alikuwa Papa kuanzia tarehe 2 au 12 Februari 1049 hadi kifo chake[1]. Alitokea Alsace, leo nchini Ufaransa[2].

Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Bruno wa Eguisheim-Dagsburg[3].

Alimfuata Papa Damaso II akafuatwa na Papa Viktor II.

Akielekea Roma kwa ajili ya kutawazwa, alikutana na abati Hugo wa Cluny na kumchukua mmonaki Hildebrando ambaye akaja kuwa Papa Gregori VII[4].

Alikuwa Papa bora kutoka Ujerumani katika Karne za Kati, akijitahidi kupambana na maovu ya wakati ule[5], ingawa kutokana na utawala wake lilitokea farakano na Kanisa la Kigiriki (Farakano la mwaka 1054)[6] .

Alitangazwa na Papa Gregori VII kuwa mtakatifu mwaka 1082.

Sikukuu yake huadhimishwa kwenye tarehe ya kifo chake[7].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  3. Coulombe, Charles A., Vicars of Christ: A History of the Popes, (Citadel Press, 2003), 204.
  4. Leo IX (Bruno von Egisheim und Dagsburg), Pope | Saints Resource.
  5. Butler, Alban, Butler's Lives of the Saints, (Liturgical Press, 2003), 176.
  6. Brett Edward Whalen, Dominion of God: Christendom and Apocalypse in the Middle Ages (Harvard University Press, 2009), p. 24.
  7. Martyrologium Romanum

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Leo IX kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.