Ponsyo Pilato

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Pontio Pilato)
Ecce Homo, mchoro wa Antonio Ciseri unaoonyesha Ponsyo Pilato alivyomtambulisha Yesu kwa watu wa Yerusalemu baada ya kumpiga mijeledi

Ponsyo Pilato (kwa Kilatini Pontius Pilatus; kwa Kigiriki Πόντιος Πιλᾶτος; kwa Kiebrania פונטיוס פילאטוס; alikuwa liwali wa kiroma katika Palestina kwenye miaka 26-36.

Anajulikana kutoka vyanzo mbalimbali, lakini hasa kwa sababu ya Injili kumtaja kama hakimu aliyempeleka Yesu kuuawa msalabani. Vyanzo vingine ni katika maandiko ya Yosefu Flavius, Tacitus na Filo wa Aleksandria.

Waandishi Wayahudi Josephus na Philo wanamwonyesha kama mtawala mkali asiyeheshimu utamaduni na imani ya wenyeji wa Palestina. Baada ya kutumia unyama katika ukandamizaji wa Wasamaria aliitwa kurudi Roma na kufika mbele ya Kaisari. Hakuna habari za uhakika kuhusu maisha yake ya baadaye.

Kanisa la Ethiopia linafuata hadithi ya kwamba aliongoka, hivyo linamheshimu kama mtakatifu.

Kadiri ya mapokeo mengine, alijiua.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ponsyo Pilato kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.