Polikarpo Mtakatifu
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu Polikarpo (takriban 69-155) alikuwa askofu nchini Uturuki.
Ametambuliwa kuwa mtakatifu kama mfiadini.
Sikukuu yake ni 23 Februari.
[hariri] Maisha
Polikarpo alikuwa mwanafunzi wa mtume Yohane na askofu wa mji wa Smirna (leo Izmir nchini Uturuki). Pengine barua kwa malaika wa Kanisa la Smirna inayopatikana katika Kitabu cha Ufunuo ilimlenga na kumsifu yeye.
Alikuwa rafiki ya Mt. Ignasi wa Antiokia ambaye alimuandikia barua maarufu.
Alikwenda Roma, Italia, kuzungumza na Mt. Papa Anicetus kuhusu maadhimisho ya Pasaka.
Mwaka 155 aliifia dini yake kwa kuchomwa moto katika uwanja wa michezo. Habari za kifodini hicho zinasifiwa kwa uzuri wake.
[hariri] Tazama pia
[hariri] Marejeo
- "Sala ya Kanisa - Vipindi vya Liturjia", Toleo la Tatu 1996, Ndanda - Peramiho: Benedictine Publications, uk.1295
| Makala hii kuhusu Mkristo huyu bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Polikarpo Mtakatifu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |