Domofupi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Parus)
Domofupi
Domofupi tumbo-jeupe
Domofupi tumbo-jeupe
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Sylvioidea (Ndege kama kucha)
Familia: Paridae (Ndege walio na mnasaba na domofupi)
Ngazi za chini

Jenasi 14:

Domofupi ni ndege wa familia Paridae. Hawa ni ndege wadogo wenye domo fupi na mkia mfupi; spishi kadhaa zina kishungi. Rangi zao si kali sana: kwa kawaida nyeusi, nyeupe, kijivu na/au kahawia, pengine buluu, njano na nyekundu. Wanatokea Afrika, Asia, Ulaya na Amerika ya Kaskazini katika maeneo yenye miti. Hula wadudu na pia mbegu na makokwa. Hulijenga tago lao ndani ya tundu mtini. Jike huyataga mayai 3-19 yenye madoa.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]